Thursday, July 23, 2015

“KIJANA NA MALENGO”


Shalom ndugu msomaji,yaani Amani iwe kwako!
Habari yako kijana? Naamini unasoma hapa ukiwa na utulivu kabisa moyoni na akili timamu kichwani!

Najisikia vizuri kusema nawe kwa habari ya “KIJANA NA MALENGO”
Kwanza natamani tuanze kwanza kwa tafakari na maana ya maneno haya mawili:
KIJANA: Ziko tafasiri nyingi kuhusu kijana ila mimi niseme tu, Kijana/Ujana ni hatua ya kati ya ukuuaji wa binadamu toka “Utoto” kwenda “Utu Uzima/Uzee”; na ndio katika hatua hii mtu anakuwa na nguvu nyingi,ari kubwa ya kufanya mambo, uwezo wa kufanya chochote na udadisi wa kutaka kujaribu kila kitu.  Kijana kwasababu anazo nguvu anategemewa nay eye mwenyewe,familia na jamii yake, nchi yake, dunia yake na hata Kanisa na Mungu wake.

MALENGO: Ni mipango, mikakati na matazamio yenye nia, yanayojenga tumaini la mwongozo wa kesho ya mtu. Malengo ni shabaha ya mbali ya kuifikia, ambayo humpa mtu ujasiri na juhudi ya kufika pale. Malengo ni ramani na barabara ya kupita kufikia hatma yako. Unaweza kutafasiri Mipango peke yake, lakini hakuna mipango wala mikakati bila Malengo na hakuna ndoto ya maana bila Malengo.

Kabla ya kuianza safari malengo huwa ni mipango tu,ila mara unapofikia mwisho wa safari hiyo, malengo huwa ni faida ya matokeo ya safari hiyo!

SASA KWANINI KIJANA NA MALENGO?

Ujana ndio hatua amabayo mtu ana nguvu ya kupanga na kutenda,na ni hatua ambayo mtu amepevuka kimajukumu na anategewa na kila amtazamaye, hususani yeye mwenyewe binafsi, hivyo ni muhimu kuwa na ndoto ama maono makubwa, si juu yake binafsi,maana huo ni ubinafsi, bali kwa ajili ya watu wengine wanaomhusu kama jamii yake, Taifa lake na kanisa kwa ujumla!
Sasa hayo maono na ndoto kubwa haziwezi kufikiwa ama kutimia kwa mara moja, ni hatua kwa hatua, na hapo ndio tunapata umuhimu sasa wa kujiwekea malengo ambayo hufikiwa kupitia mipango.

Ni Zaidi ya muhimu,kwa kijana kuweka malengo kwasababu zifuatazo;

1.       “Asiyejua aendako huwa hapotei, na kila njia aishikayo ni sahihi kwake”

Msemo huu unamaanisha kuwa bila kujua unakotaka kwenda kila njia iliyo mbele yako itakufikisha, uhalisia ni kuwa ukifuata njia yoyote utafika mahali njia inakofika na sio wewe unakopaswa kufika, huapaswi kupoteza muda, nguvu na rasilimali kubahatisha kufanya mambo, maana maisha sio bahati nasibu na wala sio mazoezi, ila ndio yanaendelea hivyo, kila sekunde ipitayo ndio imeshapita na kila hatua urukayo ndio umehsaruka, sasa ili uwe makini, uwe na hakika na safari yako kuelekea kesho yako, ni muhimu sana kujiwekea malengo, ambayo yanakuwa kama ramani yako kuifikia hatma ya matarajio yako maishani.

2.       “Huwezi kupima kipimo chochote bila kipimio, na huwezi kufananisha kitu chochote bila kifananishio”

Sijui kama ni lugha sahihi, lakini kimsingi kila kipimo kinachofahamika hapa duniani kina kifaa Fulani ambacho huitwa “kipimio” kwa mfano uzito utapimwa kwa mzani; hali kadhalika urefu,kina, ukubwa, ujazo na vinginevyo navyo vina vipimo vyake. Pia huwezi kufananisha kitu,bila kuwa na kingine cha kufananishia, yaani huwezi kusema huyu Anafanana au huyu ni mfupi ama huyu ni mnene bila kwanza kuwa na mwingine aitha halisi au kichwani mwako unayemfanisha ama kumlinganisha naye. Naam na Malengo ni kama Kipimio cha shabaha yako na kifananishio akilini mwako ambavyo vitakusaidia uwe na juhudi na nia thabiti ili ufike mahali ambapo unaweza sasa kupima uhalisia na kipimio kiitwacho malengo na kufanisha na kifananishio hicho. Ukiweka malengo ni kama unayo picha halisi kichwani ambayo bado kuifikia, na mara utakapoendelea na kufika hatua Fulani, ni rahisi kuangalia uhalisia wa jambo kama umefika ama unakaribia ile picha ya malengo iliyo kichwani mwako.

3.       Malengo kama picha ya shabaha, yatukusaidia kuamua na kupanga vema juu ya mahitaji yahitajikayo kufika pale. Yaani ukiwa na ile picha ambayo unatamani kuifikia, ni rahisi sasa kujua unahitaji nini na unamwitaji nani kwa hatua gani na kwa muda gani ili kuitimiliza hiyo nadharia ambayo sasa ni picha na iwe halisi.

4.       Malengo ni kichochezi chanya cha juhudi ya mtu kutumia sawasawa uwezo wake wa juu ili kupata matokeo bora ya kile anachokitarajia. Bila malengo mtu anaweza kubweteka na kutumia kiasi kidogo sana cha uwezo wake wa kufikiri na kutenda, na akajikuta anapoteza muda wake na nguvu zake kwa mambo yasiyoeleweka na yasiyo na tija.

Pamoja na yote hayo, malengo sio bima ya kufikia hatma ya jambo lako, unaweza ukashindwa na kuanguka mara kadhaa katika jambo hilo, naam hata ukaamua kubadilisha namna ya kufanya jambo hilo, lakini bado Malengo yanabaki kuwa dira, ama shabaha ambayo kwa njia yeyote ile lazima uifikie na labda na kuipitiliza kabisa.

Ili upange malengo vema yanaweza kufikiwa ni muhimu kuzingatia mambo yafuatayo;

i.Ni lazima Uwe na taarifa sahihi na za kutosha kuhusu jambo hilo unalolipangia malengo, na hata kama sio zote basi zile za msingi zinazokupa ujasiri wa kuamini kuwa inawezekana;

ii. Kama ni jambo la kitaalamu, basi uwe na hakika na ujuzi ulio nao, ama uwe na hakika na wataalamu ulio nao na ujiridhishe na ujuzi ama taarifa walizo nazo kuwa zimethibitishwa.

iii. Lazima uzingatie matumizi mazuri ya muda, upange mipango inayoweza kutekelezeka katika muda unaoamini unafaa, usijibane sana ukalipua na usijipe mwingi kupitiliza ukabweteka.

iv. Lazima uwe na hakika na mahitaji pamoja rasilimali zinazohitajika ili kufikia malengo yako, na hapa namaanisha zote, yaani rasilimali watu, rasilimali vitu na fedha.

v. Lazima mazingira yawe yanaruhusu bila shida jambo hilo, yaani mazingira asili pamoja mazingira ya utawala wa nchi. Lazima uwe na hakika kuwa unalotaka kufanya haligombani na mazingira wa sharia na taratibu za nchi.

Lakini pia malengo humfanya mtu azidi kujifunza na kutafuta taarifa Zaidi kuhusu jambo ambalo ameanza kulifanya, pia malengo yanamsaidia mtu kupata watu sahihi wa kushirikiana nao, mahali sahihi pa kufanya jambo kwa wakati sahihi.

Najua unayo maono na ndoto nyingi sana kijana, na unatamani kama zingetimia hata kesho, najua unatamani kuishi maisha Fulani hivi yasiyo na bugudha na unatamani kuwa akina Fulani wenye hela zao, ni sawa inawezekana kabisa kuwa vyovyote utakavyo, na Mungu ameweka uwezo ndani yako kutimiza chochote ukusudiacho kufanya, sasa ili ufike huko utakapo, kwanza imekupasa kujitambua vema na kujikubali, kuwa wewe mwenyewe halisi na wala usitamani kuwa kama yeyote yule umtamaniye, maana hata ufanye juhudi gani hautaweza; Usishindane na yeyote wala usigombane na mtu, wewe tazama mbele yako, ona ile picha kicwani mwako unayotaka kuwa, kisha panga mikakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu ambayo itakuwezesha kuyafikia malengo yako. Usitamani kufika haraka, uwe na subira na usiruke hatua wala kutaka njia za mkato, tembea hatua kwa hatua, ongeza juhudi, imarisha Imani yako na nia na kaa mahali sahihi na watu sahihi kila siku, na mimi ninayo hakika kuwa lazima utayafikia tu malengo yako siku moja.

Kijana malengo yatakusaidia kuwa na adabu na muono wa mbali katika yale uyafanyayo sasa, unataka kuwa mwandishi mzuri, jiwekee malengo ya kusoma vitabu kadhaa kila mwezi; Unataka kuwa kiongozi, jiwekee malengo ya kufanya jambo moja la kijamii kila baada ya wakati Fulani; Ama niseme unacheza mpira sawa, basi jiwekee malengo ya kucheza mpira Afrika ama duniani na anza juhudi ya zoezi sasa, Una malengo ya kuajiriwa mahali Fulani, basi anza kujifunza kidogo kidogo kuhusu watu hao, naam ukipata nafasi ya kufanya mazoezi hapo, fanya Zaidi yaw engine, kwa uaminifu na juhudi kubwa nao hawatakusahau hata iweje. Unatamani kujiajiri ama kuja kuwa mfanya biashara mkubwa duniani, ni vema, basi jiwekee malengo ya kuweka akiba na kuanza kuzungusha hela kidogo kidogo na uone kama hautayafikia malengo yako.

Najua unaweza kuwa unatamani kuwa maarufu, sijui ni kwanini na yamkini hata wewe mwenyewe hujui hasa kwanini unatamani, ila nataka nikwambie kitu kimoja tu, kama ukiwa halisi, ukiwa makini na nia thabiti katika yale uyafanyayo kwa juhudi na uthabiti mkubwa, basi uwe na hakika, kazi yako itakutangaza tu, na kwakuwa hakuna pilau nzuri ipikwayo isinukie, basi nawe kupitia hayo uyatendayo utakuwa maarufu tu, hata kama hutaki!

Mungu akubariki na kukuwezesha katika yote ufanyayo, naam na Roho wake wa Ufahamu akufundishe na kukufunulia yale yote unayohitaji kuyajua ili kutimiliza kusudi la kuishi kwako hapa duniani kwa faida yako na wote wanaokutegemea….Nenda sasa kijana ukajiwekee MALENGO, Na saa ile ikifika YAKATIMIE! Amen!



Na
 Fredy Erasto Chavala (King Chavala-MC)
(Mwalimu na Mshauri wa Vijana/ Mzungumzaji wa hadhira/Mshereheshaji/Mchekeshaji/Mwandishi na Mtaalamu wa Biashara na Utawala kitaaluma)
+255 713 883 797

Barua pepe: lacs.project@gmail.com

Monday, January 26, 2015

MAMBO MATANO NILIYOJIFUNZA KUTOKA KWA PENSELI!!

MTENGENEZAJI WA PENSELI ANAYO MAMBO 5

NIYAPENDAYO,NA HAYO NI MAFUNZO KWA PENSELI NA SISI LEO!!!

Mtengenezaji wa PENSELI aliiambia penseli haya na mimi leo ninawaambia ninyi;

1.Eeeh PENSELI popote utakapogusa utaacha ALAMA (Haijalishi ni vizuri au vibaya)
>>>NA WEWE PIA KILA UNAPOPITA MAISHANI MWAKO UNAACHA ALAMA KWA WATU.

2.Eeeh PENSELI najua unaweza kukosea mara nyingi,basi usijali,juu yako upo MFUTO ili kufuta kila alama mbaya isiyotakiwa.
>>>NA WEWE PIA NAKUAMBIA HATA UKIFANYA MAKOSA KIASI GANI,MFUTO WA DAMU YA YESU UKO JUU YAKO.....Hakuna awezaye kurudi nyuma kuanza upya,ila pale ulipo panaweza kuwa hatua ya mwanzo mpya!

3.Eeeh PENSELI,Kitu cha muhimu sana kwako ni kile ambacho KIKO NDANI YAKO(Risasi ya graphite),Hata kama uwe na umbo ama umbile lenye mapambo kiasi gani!
>>>NA WEWE PIA TAMBUA YA KUWA KUSUDI LA KUISHI NDANI YAKO NDIO MUHIMU SANA MAISHANI MWAKO KATIKA KUMPENDEZA MUNGU,YAANI LILE MUNGU ALILOKUANDIKIA na haya mengineyo ya nje ni mbwembwe tu!

4.Eeeh PENSELI Hauwezi kuandika vizuri mpaka ukubali KUCHONGWA VIZURI ili uwe sharp(sio ombi unless unataka kuwa pambo)
>>>NA WEWE LAZIMA UJUE JAMBO MOJA KUWA ILI KWENYE MAISHA YAKO UUFURAHIE MWITO WAKO,LAZIMA UKUBALI KUCHONGWA AMA KUPITIA MAGUMU ILI UJIFUNZE KUKUA NA KUKOMAA.

5.Eeeh PENSELI pamoja na yote hayo bado huwezi kuandika au kuifurahia kazi yako,ni lazima UKUBALI KUSHIKWA NA MKONO HODARI ili mwandiko au mchoro uwe bora!
>>>NA WEWE PIA LAZIMA UKUBALI KUSHIKWA NA MUNGU MWENYEWE NA KUFUATA NENO LAKE NA KILA AKITAKACHO NA HAPO NDIO UTAPONA NA KUWA NA FURAHA MAISHANI MWAKO!!!

Ubarikiwe sana kama umenielewa na ukiweza SHARE na wenzako wasome!!!

Na King Chavala MC
+255 713 883 797

Wednesday, December 10, 2014

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 5(mwisho)


Shalom!
Yesu Kristo asifiwe sana!
Naamini uliyekuwa unafuatilia mfululizo huu umejifunza mengi na kubarikiwa pia,leo katika sehemu ya tano...Kuhusu kusifu na kuabudu, kama nilivyoahidi sehemu ya nne,tutaangazia mambo mawili makubwa;

I.NAMNA UNAVYOWEZA KUFANYA IBAADA YA SIFA NA KUABUDU!!
Kumfanyia Bwana ibaada,inategemeana sana na mahusiano yenu...yaani ningeweza kuwianisha na Mama na mwanae,namna ya kumlisha inategemea sana na urahisi wa mtoto huyo kula na kushiba, mwingine hula akipakatwa,mwingine hula akiwa anaoga, mwingine akiwa peke yake,muhimu ni kuwa mtoto amekula!!
Ibaada njema ni ile inayoanzia ndani ya kilindi cha moyo kabisa kwa upendo mkubwa,hivyo unaweza kufanya ibaada hiyo kwa namna nyingi,na hizi ni chache ambazo zimewahi kutumika na watumishi mbalimbali katika Biblia!
Unaweza Kumsifu na Kumwabudu Bwana:
1.Kwa kuimba,Iwe kanisani au popote pale-na hapa inaweza kuwa nyimbo za vitabuni, tenzi au zaburi au nyimbo mpya za kutoka moyoni mwako unapotafakari ukuu wa Mungu!
2.Kwa kupiga kelele-hii inaweza kuwa kelele zisizo na mpangilio au vigelege au miluzi au kelele zenye mpangilio wa nyimbo fulani!
3.Kwa kucheza -furaha ya mdundo unaoanzia ndani na sio ilimradi tu kuna muziki,na kwa habari ya kucheza unaweza kucheza hata kama hakuna muziki wowote
4.Kwa ubunifu na kazi za sanaa-mfano uchongaji,uchoraji, uigizaji na kazi nyingine za sanaa ambazo mwisho wa siku Ni Mungu ndio anasifiwa na kuabudiwa peke yake
5.Kwa kulala -unaweza ukalala namna yeyote ile kama ishara ya kujinyenyekesha mbele za Bwana
6.Kwa kupiga magoti
7.Kwa kukaa kimya mbele za Bwana
8.Kwa Kulia
9.Kwa kucheka
10.Kwa kunena kwa lugha nyingine,ziwe za duniani au lugha za kimbinguni!
11.Kwa kuomba
.....Sasa sifa na kuabudu inawiana na kuingiliana sana na maombi japo unaweza Kumsifu na Kumwabudu Bwana kwa maombi!!
Hizo ni chache katika namna nyingi,ambazo unaweza kujidhihirisha mbele za Bwana!!
Watu wengi wamechukuliwa na sifa na kuabudu ile ya kuimba na kucheza labda na kulia kanisani kwa maombi,na ni sawa tu!
Ila jambo la pili ni

II.NAMNA IMPASAVYO KUWA YEYOTE AKAAYE MBELE KUONGOZA WENGINE KATIKA IBAADA YA SIFA NA KUABUDU!
Wengi hufanya kama mazoea au utaratibu tu wa ibaada kwasababu wameshaguliwa au wamefanya mazoezi au wanajua au wana vipaji lakini ni zaidi ya hapo,imekupasa. Kuwa moyo mnyofu na Ibaada nzuri huanzia ndani yako kwanza kabla wengine hawajapotelea katika wingu,
1.Imempasa mtu huyu kuwa mtakatifu/mtauwa na anayempenda Mungu kiasi cha kupenda kumfamyia ibaada hata akiwa peke yake kabla hata kuwa mbele za watu
2.Imempasa kuwa na Neno la kutosha moyoni mwake,sio maandiko ya kukariri
3.Imempasa kuwa mwombaji, maana imempasa kusikia sauti ya Mungu wazi wazi ili awapo madhabahuni asifanye kwa mazoea
4.Imempasa kuwa na muonekano usioleta maswali kwa watu,yaani mavazi,mapambo na hata kutembea tu.
5.Imempasa kuwa na Amani na watu maana ikiwa mtu huyo ana Ugomvi au maneno maneno na watu,ibaada hiyo haiwezi kukamilika
6.Uongo,uzinzi,Umbeya, Unafiki na udhalimu wowote ule usitajwe kwake akaaye mbele za watu!...maana sifa na kuabudu kwa mwenye dhambi ni kelele mbele za Mungu!
7.Imempasa kuwa mnyenyekevu na aliye jaa hekima,na asiyejaribu kujitutumua au kujiona ni yeye na.bila yeye uwepo ule usingeshuka!
Lazima umaarufu, vyeo,elimu na hadhi viwe chini ya Utukufu wa Mungu,hivyo yeyote akaaye mbele za watu ajue kabisa kuwa yuko hapo kwa ajili ya Kumsifu na Kumuabudu Mungu tu na sio kuonekana!!
Mungu Roho mtakatifu akusaidie sote kuelewa sana zaidi ya maandishi haya,ili ibaada zetu za sifa na kuabudu, ikiwa ni za binafsi au mbele ya watu zipate kibali mbele za Mungu!
Mungu akuwezeshe na Mungu akunyenyekeshe ewe Mwabudu!!
Mpaka hapa Nimemaliza kwa habari ya Kusifu na kuabudu na ninayaacha kwako wewe kujifunza na kufundisha na kushare na wengine pia!!
*Najua utakuwa unajiuliza mbona hamna mistari ya Biblia,ndio! sitaki watu wanaokariri Nataka wanaoelewa!!!
Mungu akubariki sana wewe rafiki yangu!!
*Karibu sana katika Ulimwengu wa Kusifu na Kuabudu,kwa roho na kwa akili kwa kupenda!!

***MWISHO***
(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 4


Shalom wana wa Mungu!

Wajoli na Wajeuri wa Bwana!
Tumekuwa na mfululizo wa kupendeza kuhusu sifa na kuabudu,na tangu tumeanza leo ni sehemu ya nne kati ya tano...na leo natamani kuzungumzia "Kwanini Sifa na kuabudu maishani mwetu" yaani muunganiko wa sifa na kuabudu na hatma za maisha yetu!
*Najua wengi tunajua Kusifu na kuabudu ni sehemu ya ibaada mbalimbali makanisani na ndio maana watu huanza kwa maombi,sijui matangazo kisha Kusifu na kuabudu, neno,sadaka na mengineyo Ila leo natamani nikujuze kuwa sifa na kuabudu ni zaidi ya hapo!!
Kusifu na kuabudu ni ibaada endelevu kila siku na kila mahali na kwa kila namna!
Ile ifanyikayo kanisani ni namna ya pamoja ya Kusifu na.kuabudu kwa upamoja na kwa utaratibu tuliojiwekea na kama watu wakibaki na picha hiyo pekee hawatafanya ibaada hiyo kwa ukamilifu!!! 

ZINGATIA UKWELI HUU!!
Kila mtu ameubwa kwa kusudi maalum hapa duniani na kila mtu amepewa uwezo fulani halisi unaomwezesha kufanya mambo yale yampasayo kwa urahisi kuliko yeyote mwingine(Yaani kwa mfano mimi sijitahidi kusheresha au kuchekesha maana ipo ndani naturally) na.uwezo huo huitwa kipaji na wazungu huongea kwa maringo zaidi "Gifts & Talents".....na kwa ujumla wake woote mambo haya ili tumwabudu Mungu!
Sasa kama tuna majukumu ya kufanya na hayo yote ni kwa ajili ya Kumwabudu Mungu na kuyafanya majukumu hayo ndio kuishi kwenyewe...tunaachaje kumwabudu Mungu??
Ile hali ya kujua kuwa hakuna jambo unaloweza kufanya kwa akili yako na uwezo wako binafsi na ule ukweli kuwa yote ufanyayo ni kwa utukufu wa Mungu....itakulazimu kuabudu tu,isipokuwa kama umeamua kuwa na Kiburi cha uzima na kujiona kama umejiumba mwenyewe!!
"Katika sifa Mungu hushuka" naamini umewahi kusikia sentensi hiyo Ila unadhani ni kwa ajili ya ile sifa ya kanisani pekee...Je hujawahi kusikia wale watu wa kale waliowahi kushinda vita kwa sifa?? Popote ambapo Yesu anasifiwa lazima uwepo wake uwe Kamilifu.... Sasa ukitaka mambo yako yaende sawia na kwa Ushindi lazima ukubali tu kujumlishia na Ibaada ya sifa na kuabudu!!

Kusifu na kuabudu ni kama vile kusema....MUNGU NI WEWE PEKE YAKO,HAYA YOTE NI YAKO,SHUKRANI TUKUZO NA SIFA ZOTE NI ZAKO,UMETUPA HIVI VYOTE KWA UTUKUFU WAKO,AHSANTE JEHOVA MAANA NI WEWE!!
Yaani kwamba sio kwa uwezo wako wala akili yako bali ni kwa Neema ya Mungu tu!!
Kusifu na kuabudu ni wakati wa shida na wakati wa raha,ukiwa na kusanyiko na hata ukiwa peke yako,ukiwa nyumbani na hata ukiwa mbali,kwa mavazi,muonekano, kelele, kula,kuongea,kufanya kazi na hata katika kujifurahisha!!
Muhimu kujua kuwa Umeumbwa ili umuabudu Mungu,utafundishwa kuwa mtumishi ama kuishi hatma yako au utafunzwa kuwa na ndoto au kuacha Alama itakayodumu ni sawa kabisa lakini msingi wa yote haya ni ili Mungu atukuzike..... Watu wamjue Mungu,waupokee Ufalme wake na wamuishi yeye....na hapo Ndio tunasema Maisha ya Ibaada,na.hiyo ibaada ndio Kusifu na Kumuabudu!!
Unaweza ukachoka Kumsifu alivyo mwema maishani mwako lakini kila uonapo watu wanakufa, wengine wanaumwa na hawa wapata shida....na hayo yawapatayo wenzio wewe huyashuhudii basi choka salama....na ukimjua Mungu sawasawa kuwa yeye hata nini kitokee duniani hakibadilishi Umungu wake...na kama ukijua ni baba yako,na AHADI zake kwako ni za milele,hutaacha kumuabudu leo kwasababu una mashida na machangamoto....Ila utamwabudu tu kwa kuwa yeye ni Mungu na tumaini lako la kesho maana ni hakika na Amina!
Mungu ni mwaminifu sana mara nyingine ni kiburi tu ndio huwa kinatufanya tumsifu na kumuabudu sana aitha tukiwa tuna vingi au tukiwa hatuna basi tunamlilia, na huo kwa hakika ni utoto!!
Basi Mungu akusaidie kuwa na maisha ya Kusifu na Kuabudu kila siku, kila wakati na kila mahali bila kujali nini wala nini na hakika uwepo wa Mungu hautapungua maishani mwako!!!
Kabla ya saa ile ya Agano nitamalizia sehemu ya tano na ya mwisho kwa habari ya mambo makubwa mawili;
i. Namna ambazo unaweza kufanya ibaada ya sifa na kuabudu
ii. Mambo yakupasayo kuzingatia uwapo mstari wa mbele katika kuwaongoza wengine katika sifa na kuabudu!!
Ahsante Bwana Yesu kwa kila asomaye na kuelewa somo hili,lisaidie Kanisa lijue kina na msingi wa Ibaada kuwa ni SIFA NA KUABUDU....maana hata Malaika, maserafi, makerubi,wazee 24,wenye uhai wa nne na Sisi watakatifu tuliyo duniani na hata saa ile ya mwisho kule mbinguni biashara ni moja tu "KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU"
(Usiache kushare kwa marafiki zako)

+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 3


Shalom ndugu yangu!
Naamini unaendelea vema na maisha yako na ninambariki Mungu sana kwa ajili yako na nimemwomba roho mtakatifu akusaidie kuendelea kuelewa somo hili!
Mara ya mwisho niliongelea mambo mawili makubwa kwanza ni Lazima Mtu anayetaka Kumsifu na.kumuabudu Mungu kweli lazima awe na uhusiano naye thabiti na pili katika sifa na kuabudu sio wewe au Kanisa au chochote kuinuliwa zaidi ya Mungu mwenyewe!
...Na nikaacha swali....JE NI VIUNGO VIPI HULETA UTAMU WA KUSIFU NA KUABUDU!!
Basi ninamshukuru sana Mungu kwa ajili yako na natamani niseme nawewe kwa habari ya uzuri wa sifa na kuabudu!
Sisi huwa tunadhani uzuri wa sifa ni Muziki(Melody),nyimbo tuzipendazo Sisi, mavazi yetu,mitetemeko ya waongoza sifa,machozi labda na mihemuko na hapo tunaweza kuruka na kucheza sana lakini hata kama Hayo yote huwepo au ni muhimu Ila msingi wa Utamu wa sifa na kuabudu ni haya yafuatayo;
1.Ibaada ya sifa na kuabudu yenye Utamu mbele za Mungu ni ile inayofanywa na Moyo wa kumpenda yeye,moyo Safi na wenye nia thabiti ya Kumsifu na Kumuabudu!!
2.Siyo nyimbo uzipendazo wewe ndio zinaleta utamu wa sifa mbele za Mungu,sio upendazo wewe maana sio kwa ajili yako Ila kwa ajili yake mwenyewe.... Ingawa ukizama sana utagundua kuwa kile roho mtakatifu anataka na wewe unaingiwa kupenda kile atakacho!!!
*Sasa natoa tahadhari tu.... Acha ubinafsi wa kutaka Kusifu na kuabudu kwa matakwa yako Ila msikilize sana roho ili mara zote umeona wingu lake!
3.Na tatu ni ile hamu ya kumtaka Mungu Atukuzike katika sifa na kuabudu ndio inafanya moyo wako uwe mnyenyekevu na kwa hakika Mungu ajidhihirishe na sio kuwa na hamu ya kutaka kusifiwa au kupongezwa baada ya uwepo kudhihihirika!
*Unajua Mungu akisifiwa hushuka lakini ile hamu yako ya kumuona Mungu zaidi na sio Kiasi wewe uonekane kama wewe ndio huwa unasifu na kuabudu mpaka uwepo unashuka!
4.Na mwisho;Ili ibaada ya Kusifu na kuabudu Iwe na tamu....Ni mara zote ikiwa unafanya ibaada ya sifa na kuabudu lazima uwepo umoja kati ya moyo wako au roho yako na nafsi yako na mwili wako lakini pia ikiwa mnafanya ibaada mkiwa wengi basi iwepo nia moja na mara zote muonekano wako, mkao wako na mavazi yako,yakupe nafasi ya kuwa na utulivu mbele za Mungu.... Haiwezekani ibaada ya sifa na kuabudu Iwe tamu wakati moyo na akili yako na nafsi yako havina ushirikiano....na huwezi kuwa huru kufanya chochote mbele za Mungu kama kucheza,kulia au kurukaruka hali mavazi yako yana thamani kuliko hiyo ibaada kiasi huwezi hata kupiga magoti,huwezi kucheza kwasababu ya hadhi au cheo chako au mavazi yako yanakubana au yanawakwaza wengine!!
Natamani roho mtakatifu akusaidie kuelewa haya,maana ibaada.ya sifa na.kuabudu ni ya Mungu mwenyewe na wakati wote kumbuka "ALITUUMBA ILI TUMUABUDU"
Basi wakati mwingine nitaendelea kuzungumzia kwa kina "Kwanini Sifa na kuabudu maishani mwetu? na nini uhusiano wake na makusudio ambayo Mungu alituumba nayo"


(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 2



Shalom!
Naamini unaendelea vema hata leo,kama ulisoma sehemu ya kwanza(na kama bado nenda kwa wall yangu usome post yenye kichwa kama hiki )...nilianza kwa kujenga msingi wa Kusifu na kuabudu!
Na nikamalizia kwa swali...Nani mwabudu Mungu wa Kweli na imempasa kufanyaje???
LEO
Natamani kusisitiza mambo makubwa mawili tu katika sifa na kuabudu!!
Yaani haya yakae moyoni na kichwani mwa yeyote anayetamani kuugusa moyo wa Mungu kwa sifa na kuabudu,nayo ni haya;
1.LAZIMA KUMJUA NA KUMFAHAMU SANA HUYO MUNGU NA KUWA NA UHUSIANO NAYE.
Huwezi kufanya ibaada yeyote kwa Mungu ikawa ya maana kama unamsikia tu na humfahamu kabisa....imetupasa kumjua tena kumjua zaidi,tena kuwa na uhusiano naye wa karibu....maana kwa Kadri unavyomjua zaidi ndivyo unazidi kumpenda yeye na Kumsifu na kumuabudu kweli!....na hapo Ndio maandiko yanasema "Kusifu kwawapasa wanyofu wa mioyo"...Okey ngoja nitoe mfano huu,Kumsifu Mungu wakati hata hamna uhusiano wa karibu na sawa na kuona mjini gari aina ya Hammer ambayo iko mitaani kwenu na ukaanza kuwasimulia wenzio..."Oyaaa unaona ile hammer,yaani nyumba yetu hii unapita mtaa mmoja ndio nyumba ya mwenye gari ile aisee,yaani ile gari kali kishenzi yaani duh,Nyie Acheni tu mtaa wetu mambo Safi hahaha" sasa hapo wakikuuliza ni Tsh ngapi au umewahi kupanda au anakufahamu unabaki tu Aaah mmmm Oooh...Acha bwana hilo sio lenu, jivunie chenu...JIVUNIE MUNGU MAISHANI MWAKO,SIO KUMSIKIA TU!!
2.LAZIMA MUNGU PEKE YAKE NDIO AINUKE(AWE MAARUFU)
Yaani katika sifa na kuabudu usijitahidi kujiinua au kutaka kuonekana wewe au timu yenu au mchungaji wenu au Kanisa lenu Ila Mungu pekee Ndio wakuinuliwa!!
Kuna ukuta mwembamba sana kati ya kutafuta sifa na umaarufu au kujiona na unyenyekevu wa kutaka Mungu pekee Ndio aonekane!!
Tena sio kwa maigizo bali toka moyoni... Na ukiwa na moyo wa unyenyekevu utashangaa una Amani tele hata uende wapi au watu wawe kumi tu au vyombo visiwepo au sare zisiwepo hata usipopewa maji au nauli na popote ulipo kwa kuwa umeamua kumfanyia Mungu ibaada basi utashangaa sana udhihirisho wa nguvu za Mungu!!!
Tabia za kuonyeshana na watu ufundi wa Sauti au kucheza na kusahau kuwa malengo ni kumuabudu Bwana basi hapo ibaada yote huwa sifuri maana tumejitwalia utukufu machoni pa watu.
(Ila pia haimanishi pia kuwa sifa na kuabudu vinapaswa kufanyika ovyoovyo..ustadi unahitajika mno)
Mungu awasaidie sana wote mnaokaa mbele kuwaelekeza watu au kuwaongoza uweponi mwake ili Mjue hamfanyi kwa ajili yenu Ila.kwa ajili ya Mungu!!!
.....Je ladha ya Kusifu na kuabudu inatokana na.viungo gani???

(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797

KUHUSU KUSIFU NA KUABUDU-Sehemu ya 1


Naamini uko poa na unaendelea vizuri!!
Naamini bado una akili timamu na unajielewa zaidi una hofu ya Mungu ndani yako (Kama sivyo basi hapa kwako ni pagumu)
"KUSIFU" na "KUABUDU" ni ibaada kamili mbele za Mungu,msingi wa ibaada zote na inayopaswa kufanywa kwa makini,ustadi na furaha tele kwa ajili ya Mungu na Ibaada hiyo inawapasa wanyofu wa mioyo!!
KUSIFU-Ni ibaada ya kushukuru,kushangilia, kumkubali,kumsifia,kumwadhimisha,na kumtukuza Mungu kwa matendo yake makuu aliyo,anayo na tunayoamini anaendelea kututendea.
Unaweza kumfanyia sifa kwa yale aliyoyatenda kwa wengine au hata ujumla wa matendo yake maishani mwetu!
*Mara nyingi imetafasirika kuwa sifa ni nyimbo za haraka na shangwe Ila natamani Mjue sifa zaidi ni maudhui na makusudi ya moyo wa mtaa sifa!!
KUABUDU-Ni ibaada ya unyenyekevu,heshima na adhama. Kwa Mungu kukubali,kutii na kumuadhimisha kwa sifa na tabia zake...Hapa haijalishi amefanya chochote kwako au hajajibu maombi yako kama uonavyo Ila anaabudiwa kwa JINSI ALIVYO!
Niweke msisitizo hapa yaani hata kama Huna kazi,umefeli au umeachika bado Yeye ni Mungu tu na Ni mtakatifu tu na Ni mwema tu!!!
*Pia kwa wengi imetafasirika kuwa kuabudu ni nyimbo za taratibu,za kulia na hisia kali...lakini Nataka Mjue kuwa kuabudu ni Maudhui na mwelekeo wa Moyo!!
Sasa Nani ni mwabudu halisi na Anayemsifu Mungu kweli???
Na imempasa nini mtu huyooo....??

(c)King Chavvah, 2014
+255 713 883 797