Showing posts with label News. Show all posts
Showing posts with label News. Show all posts

Wednesday, February 19, 2014

MWALIMU CHRISTOPHER MWAKASEGE JANGWANI TENA!!!

HII NI SEMINA YA NENO LA MUNGU KWA AJILI YA WATU WOTE,BILA KUJALI DINI WALA MADHEHEBU YAO, NJOO ULE NENO NA UKUE KIROHO!!
HUU NI MWAKA MWINGINE TENA NA HII NI SEMINA YA KWANZA KWA DAR,PANGA KUTOKUKOSA!!
HAKUNA KIINGILIO CHOCHOTE!!!

Semina itakuwa ikirushwa moja kwa moja kupitia WAPO Fm (98.1) na UPENDO Fm (107.7)

Thursday, February 13, 2014

WASANII "KUREJEA MADHABAHUNI" NDANI GOSPEL ARTISTS BREAKFAST!!! 22/02/2014

SHALOM!
Kwa mara nyingine tena Ikiwa ni ukurasa wa kwanza wa msimu wa pili na mara ya kwanza kwa 2014, Chavala Ideas Platform (Mahali yanapozaliwa mawazo mapya na makutano ya mawazo yanayotekelezeka) kupitia Wavuti ya Kikristo Gospel Standard Base wamekuandalia tena Staftahi maalum kwa ajili ya mwili wako na nyingine kubwa zaidi kwa ajili ya roho yako wewe ulipewa kipawa na unatumika madhabahuni kwa Bwana iitwayo "GOSPEL ARTISTS BREAKFAST"
Chai hii maalum kwa ajili ya waimbaji wa aina zote za nyimbo za injili,wachezaji,wapiga vyombo,wazalishaji,wasmbazaji,watangazaji,wachekeshaji,waigizaji na kila mwenye kipawa chake anachokitumia madhabahuni itanyweka pale WORDALIVE CENTRE-Sinza Mori, Jumamosi ya tarehe 22/02/2014 Kuanzaia saa 2 asubuhi mpaka 5:59 asubuhi!
Maada au msingi wa chai hii utakuwa ni juu ya wasanii wa injili "KUREJEA MADHABAHUNI" na Mchungaji na mwanamuziki wa siku nyungi Rev.DAVID NKONE atatuhudumia!

Hii sio fursa ya kukosa na sio kwa ajili ya mtu fulani tu maalum,bali ni kwa ajili ya kila anayemaanisha kutumika madhabahuni!
Hakuna Kiingilio na ukiwahi utafanya jambo la maana zaidi!!!

Chai hii inandaliwa na MODERN EVENTS CEREMONERZ
Kwa kusirikiana na WordAlive Centre na

Imedhaminiwa na
1.Great Potentials Ltd
(......Living your Dreams by your potential!!)
2Quality Vision Picture

(Quality vision pictures inafanya Gospel Videos.na sasa kwa watu  20 wa mwanzo kuna ofa maalumu kwa mawasiliano wafike officen Kimara. 0715416961,na 657295614)

NJOO UONGEZA MAARIFA,NJOO UCHANGAMOTISHWE NA NJOO UFAHAMIANE NA MARAFIKI WENGINE,NI MATUMAINI YANGU KUWA HAUTAKUJA PEKE YAKO!!!

0713 883 797

Saturday, January 4, 2014

HERI YA MWAKA MPYA 2014!!!!

Shalom!!!
Habari zenu wapendwa wasomaji wa blog hii!!
Tulikuwa kimya na sasa tumerudi tena na huu ni msimu mpya!
Naamini mmekuwa na wakati mzuri wakati wa Sikukuu ya Noeli na hata shamrashamra za kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka 2014!

NENO LA KINABII KWA 2014;
*PAMOJA NA MISUKOSUKO MINGI SANA ITAKAYOKUWEPO MWAKA HUU KISIASA,KIJAMII, KIUCHUMI NA KIIMANI BADO WALE WAMTUMAINIO BWANA WATAUONA MKONO WA MUNGU....NAAM HUU NI MWAKA WA KIBALI KIKUBWA KUTOKA KWA BWANA (A YEAR OF MEGA FAVOUR)
>>>NA KAMA VILE MUNGU ALIVYOWASHINDIA WANA ISRAELI NA KUWAVUSHA BAHARI YA SHAMU,NDIVYO ITAKAVYOKUWA KWA WANA WA MUNGU!!!

*LAKINI PIA NI MWAKA WA KUVUKA KWENDA NG'AMBO YA PILI...A YEAR OF CROSSING OVER!!!

TUNAYO MENGI YA KUJIFUNZA NA KUSHIRIKISHANA HAPA!
TAFADHALI USIONDOKE HAPA NA KAMA BADO HUJAJIUNGA NA BLOG HII BASI JIUNGE SASA!!

KWA NIABA YA TIMU NZIMA YA "GOSPEL STANDARD BASE" NINAKUTAKIA KILA BARAKA NDANI YA MWAKA HUU NA MAFANIKIO MENGI SANA!!

KAA MKAO WA KUMSIKIA BWANA WAKATI WOTE!

Fredy E. Chavala
President
(c)2014

Wednesday, November 20, 2013

JUMAPILI HII HAPATATOSHA CCC-UPANGA KWA UJIO NA MOTO MPYA WA CHRISTINA SHUSHO!!!!!

KAMA HABARI HII HAIJAKUFIKIA BASI NAOMBA NIKUJUZE RASMI!
MWANAMAMA ANAYETAMBA NA MAHADHI YA KIPEKEE KATIKA MUZIKI WA INJILI TANZANIA NA AFRIKA MASHARIKI,IKIWA TU BAADA YA KUJINYAKULIA TUZO YA MWANAMUZIKI BORA WA INJILI AFRIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI KWA 2013,SASA ANAKUJA KIVINGINE,ANAKUJA UPYA,NDIO AMEAMUA KUHAMA KABISA TOKA KUIMBA KWA KUTUMIA CD MPAKA KUIMBA MOJA KWA MOJA......NI JUMAPILI HII NDANI YA UKUMBI WA CCC-UPANGA!
JUKWAANI ATAIMBA PAMOJA NA BAHATI BUKUKU,UPENDO KILAHIRO,JOSHUA MLELWA,AMANI KAPAMA,PAUL CLEMENT,THE VOICE ACAPELLA PAMOJA NA KINONDONI REVIVAL CHOIR!
MAJIRA YA SAA NANE GETI LITAKUWA WAZI NA SAA TISA TAMASHA LITAANZA RASMI,KAMA WEWE NI MGENI MAHALI HAPO BASI FIKA POSTA MPYA SAA NANE NA HAPO UTAPATA GARI MPAKA UKUMBINI KWA BEI YA KAWAIDA!
UTAKUWA SEHEMU YA HISTORIA HII KWA KUCHANGIA KWA KUNUNUA TIKETI TSH 10,000/= KAWAIDA,20,000/=VIP NA 3000/= KWA WATOTO!
NI VIZURI KUPATA TIKETI YAKO MAPEMA PALE SILVERSPOON-MLIMANICITY,MWENGE-PUMA KITUO CHA MAFUTA NA STEERS-POSTA,INGAWA HATA MLANGONI ZITAKUWEPO!
ZINGATIA KUWAHI,ZINGATIA KUWATAARIFU WENGINE NA KWA JAMBO LOLOTE LA ZIADA BASI USISITE KUWASILIANA KUPITIA
0713883 797 AU 0713 905 118

Tuesday, November 5, 2013

KWA MARA YA KWANZA "CHRISTINA SHUSHO" KUIMBA LIVE KATIKA TAMASHA LAKE LA "NATAKA NIMJUE" 24/11/2013 PALE CCC-UPANGA!!!!

Shalom Tanzania!
Baada ya kimya kirefu, mizunguko mingi ya ndani na nje ya nchi kihuduma, Hatimaye Mwanamama, Mtumishi, Mwimbaji alijinyakulia tuzo ya Uanamuziki bora wa nyimbo za injili Ukanda huu wa Afrika Mashariki, CHRISTINA SHUSHO, Sasa amekuja na jambo kubwa la kipee na hili ni TAMASHA LA KUSIFU NA KUMWABUDU MUNGU!
katika TAMASHA hili lililopewa jina "NATAKA NIMJUE", CHRISTINA SHUSHO ATAIMBA LIVE (BILA KUTUMIA CD) na atasindikizwa na Waimbaji kama
1.BAHATI BUKUKU
BAHATI BUKUKU

HUYU NI MWANAMUZIKI ANAYETAMBA NA ALBUM YAKE MPYA KWA SASA IITWAYO "DUNIA HAINA HURUMA"
2.UPENDO KILAHIRO
Pia Vijana wanaochipukia kwa sasa, hapa ninamzungumzia PAUL CLEMENT na mpiga DRUM maarufu mjini na mwimbaji AMANI KAPAMA
PAUL CLEMENT

AMANI KAPAMA
Mkongwe na Muasisi wa Live JOHN LISSU Ambaye amefanya LIVE RECORDING yake kipindi sio kirefu lilichopita mwaka huu!
CHRISTINA SHUSHO & JOHN LISSU

JAMBO KUBWA ZAIDI NI KUWA TAMASHA HILI LITAONGEZEWA VIONJO VYA kwaya ya KINONDONI REVIVAL, watu waliouvuma sana na ule wimbo wao wa "KWANINI UNATAKA KUJIUA?" pamoja vijana wa THE VOICE Acapella!
KINONDONI REVIVAL CHOIR

THE VOICE
TAMASHA HILI LINATARAJIWA KUFANYIKA KATIKA UKUMBI WA CITY CHRISTIAN CENTRE, TAREHE 24/11/2013 KUANZIA SAA NANE MCHANA MPAKA MOJA JIONI KWA VIINGILIO VYA TSH 10,000(Kawaida) na 20,000 (VIP)
Tiketi zinapatikana SILVERSPOON-mlimani city
Kituo cha MAfuta Mwenge-PUMA,kwenye baadhi ya makanisa pamoja na
Banana kwa Giddo
CCC-Mlangoni.....Kumbuka Usafiri kutoka Posta utakuwepo kuwaleta watu tamashani kwa wale wasiopafahu.

Na King Chavala-MC
Publicity & Protocal Manager

KWA MAELEZO ZAIDI
Piga 0713905118 au 0713883797

Monday, November 4, 2013

NEEMA MBISE KUZINDUA ALBUM YAKA YA SAUTI NA VIDEO TAR 17 NOV MOSHI MJINI!!!

MWANAMUZIKI WA INJILI ANAYECHIPUKIA, ANAYEVUMA SANA PANDE ZA KASKAZINI MWA TANZANIA, BAADA YA KUREKODI SAUTI NA KUFANYA VIDEO YA ALBUM YAKE IJULIKANAYO KAMA "SINA CHA KUKUPA"
HATIMAYE YUKO TAYARI KWA AJILI YA KUIWEKA WAKFU AMA KUZINDUA KAMA WENGI WALIVYOZOEA KUITA...TAMASHA HILI KUBWA LA KIPEKEE LINATARAJIA KUWAKUSANYA WAKAZI WA MOSHI NA ARUSHA PAMOJA NA VITONGOJI VYAKE, NEEMA MBISE ATASINDIKIZWA NA WAIMBAJI KAMA VILE
1.AMBWENE MWASONGWE
2.AMBELE CHAPANYOTA
3.LEMBO JUNIOR
4.DANIEL SAFARI
5.GRACE WAGANA
6. ANTONY FRANK NKONDOLA
7.ARUSHA MASS CHOIR NA
8.THE SPRING OF PRAISE
NA WENGINE WENGI BILA KUMSAHAU MISE ANAEL ANAYEABUDU NA KUSIFU KWA KUTUMIA KIFAA KIITWACHO SAKSAFONI!

TAMASHA HILI LITAFANYIKA JUMAPILI YA TAREHE 17/11/2013 PALE UKUMBI WA MR PRICE CITY MOSHI-MKABALA NA TANESCO, KUANZIA SAA NANE MCHANA

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO, MHESHIMIWA LEONIDAS GAMA NDIYE ANAYETARAJIWA KUWA MGENI RASMI NA TAMASHA HILO LITAENDESHWA NA MSHEREHESHAJI NA MCHEKESHAJI MAARUFU TANZANIA, KING CHAVALA-MC TOKA DAR ES SALAAM!!

NI MUHIMU SANA NA WEWE KUWA SEHEMU YA TAMASHA HILI....TIKETI NI 2000 TU KWA WATU WAZIMA NA 1000 KWA WATOTO!

NEEMA MBISE NI MWIMBAJI WA MAZINGIRA YETU YA NYUMBANI...HEKO WATU WOTE WA MOSHI TUJITOKEZE KUMPA MKONO WA KUMTIA MOYO BINTI YETU!!

GOSPEL STANDARD BASE INAWATAKIENI MAANDALIZI MEMA NA TAMASHA JEMA!!!

Tuesday, October 29, 2013

ANZA NOVEMBA KWA KUMSIFU MUNGU!!!

NI MUHIMU SANA KUIWEKA HII KATIKA RATIBA ZAKO!!
ANZA MWEZI NOVEMBA KWA SIFA NA KUABUDU MBELE ZA BWANA UKIWA NA TIMU NZIMA YA NEXT LEVEL PALE CITY CHRISTIAN CENTRE-UPANGA-MKABALA NA CHUO KIKUU CHA MZUMBE!!
MUNGU AKUBARIKI!!

KILA MTU NI LAZIMA ASOME KITABU HIKI...."KUSUDI LA MAJIRA YAKO!!"

USIJARIBU HATA KIDOGO KUKOSA KUSOMA KITABU HIKI CHA AJABU NA CHENYE MENGI YANAYOKUHUSU WEWE,MAANA NI MUHIMU SANA KILA MTU KUTAMBUA KUSUDI LA MAISHA YAKE!!
HAKUNA JAMBO HATARI ZAIDI DUNIANI ZAIDI YA KUISHI BILA KUJUA KUSUDI LAKO NA MBAYA ZAIDI NI WALE WAJUAO MAKUSUDI YA MAISHA YAO LAKINI HAWAJUI MAJIRA NA NYAKATI YA KUTIMILIZA YALE YAWAAPASAYO KUFANYA!!

FRED D. MSUNGU, CHURCH BOY AMEKUBALI KUTUMIWA NA BWANA NA KUAMUA KUANDIKA KITABU HIKI KIZURI SANA,NI MUHIMU UJIPATIE NAKALA YAKO NA UISOME NA KUIELEWA NA MUNGU AKUBARIKI UNAPOCHUKUA HATUA HIYO!!

KWA MAELEZO ZAIDI,WASILIANA NA MWANDISHI KWA 0653318117

Imedhaminiwa na GoStaBa
+255 713 883 797

Saturday, October 26, 2013

HATIMAYE MBUYU MKONGWE (SAMUEL SASALI) UMEANGUSHWA NA DK MILEMBE MADAHA LEO 26/10/2013!!!

CERTIFIED MR SAMUEL AND MRS MILEMBE SASALI
SASA HAWA NI MUME NA MKE RASMI NA HIVYO NDIO VYETI VYAO VYA NDOA!!
NA HIYO HATUA HAPO JUU ILIFIKA BAADA TU YA KIAPO CHA KILA MMOJA KWA MWENZAKE PAMOJA NA PETE YA AHADI YA NDOA NA KUTUNZA KIAPO HICHO
 VAA PETE HII,IWE ISHARA YA AGANO LANGU KWAKO.....
 VAA PETE HII.....
GROOM'S MEN PAMOJA NA SAMUEL SASALI

MAIDS KUMPAMBA MILEMBE
KULIKUWEPO GROOM'S MEN NA MAIDS 30 KUIPAMBA HARUSI HII YA PAPAA SEBENE!
WALIINGIA KWA FURAHA SANA NA KILA MMOJA ALIFURAHIA UCHANGAMFU WAO

MR SAMUEL AKIONGEA NA KUMSIFIA MKEWE
MRS MILEMBE MADAHA WA SAMUEL AKIONGEA
TUKAPATA KUSIKIA SAUTI ZAO,WAKASEMA NA HATIMAYE WAKAPUMZIKA KIDOGO KABLA YA KUANZA ZOEZI LA KEKI!
MR & MRS SAMUEL AND MILEMBE SASALI
HATIMAYE WALIKATA KEKI NA KULA NA

KIPEKEE WALITOA ZAWADI YA KEKI KWA WATU WAO KADHAA MUHIMU SANA, AMBAO WAMEKUWA MSAADA KWA KILA MMOJA WAO NA KWA MAHUSIANO YAO.....BAADHI YA WALIOPEWA ZAWADI YA KEKI NI PAMOJA NA WAZAZI WA PANDE ZOTE MBILI,
 MILEMBE ALIPELEKA UKWENI...
NA HUKU PIA VIVYO HIVYO!

KAMATI YA MAANDALIZI,MARAFIKI HURU,AFLEWO TEAM,DK PARVINA,PROSPER MWAKITALIMA,APOSTLE ONESMO NDEGI, LINDA TEMBA NA DK.HURUMA NKONE, MCHUNGAJI ALIYEFUNGISHA NDOA HIYO!!
KEKI KWA MCHUNGAJI NA MKE WAKE

KEKI KWA PROSPER MWAKITALIMA

KEKI KWA DK PARVINA
HATIMAYE WATU WALIKUJA KUMPONGEZA KWA KUCHEZA NA KUMRUSHA JUU SANA...
NA BAADA YA HAPO MENGI YALIENDELEA,KAMA VILE KUONA SHORT DOCUMENTARY NA HATIMAYE CHAKULA,NA HAPO WALITUMBUIZA THE VOICE,SAMWEL YONAH, AMANI KAPAMA, BOMBY JOHNSON PAMOJA NA KING CHAVALA-MC NA KIBAO MAALUM KABISA KWA MAHARUSI "SAMILEMBE"
KING CHAVALA-MC
WATU WALIKUWA WAKITOA ZAWADI MLANGONI,LAKINI KUNA BAADHI YA WATU AU MAKUNDI MAALUM YALILAZIMIKA KUPELEKA MBELE ZAWADI ZAO.
KAMATI YA MAANDALIZI ILIENDA MBELE KWA KUCHEZA KAMA HIVI
CHRISTIAN BLOGGERS NAO HAWAKUBAKI NYUMA KATIKA KUMPONGEZA MWENZAO!
"SAMILEMBE"

HATIMAYE BAADA YA YOTE WALIPIGA PICHA NA KUONDOKA KUELEKEA HUKO AMBAKO HAKUNA AJUAYE NA WAO HUJUA TU WAKISHARUDI!!

SHUKRANI NYINGI SANA KWA KAMATI YA MAANDALIZI  NA KILA ALIYEHUSIKA KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE KUFANIKISHA JAMBO HILI,AHSANTE SANA MWENYEKITI NOEL TENGA KWA KUKUBALI KUTUMIKA KUBEBA JUKUMU HILI!

KWA NIABA YA TIMU NZIMA CHA YA CHAVALA MEDIA, TUNAWATAKIA KILA LAKHERI NA MAISHA MAREFU SANA YENYE FURAHA NA AMANI NA UPENDO WA KWELI WATU HAWA MUHIMU SANA KWETU,AMEN!!

IMEANDIKWA NA 
King Chavala MC
+255 713 883 797

Monday, September 30, 2013

JOHN LISSU KUANDIKA HISTORIA YA MUZIKI WA INJILI TANZANIA TAR 06/10/2013!!!



UKO HAPA DVD LIVE RECORDING
 NA JOHN LISSU,
06/10/2013,CCC-UPANGA, DAR ES SALAAM, TANZANIA.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE;
SALAM TANZANIA!

Shalom Dar es salaam, Shalom Tanzania!
Ndugu wanahabari na watanzania wote kwa ujumla!
Naamini tuko salama na tunaendelea na shughuli zetu za kila siku alizotupatia Mungu wa mbinguni, tumshukuru Mungu sana kwa Amani na utulivu aliotupa na tuendelee kumuomba ili atuepushe na kila aina ya dhahama na uharibifu wa Yule adui!
Kama tulivyosikia hivi karibuni, yale yaliyotokea nchi jirani ya Kenya, kwa hakika tunawapa pole sana kwa mkasa huo, pole kwa wale waliowapoteza wapendwa wao na wale waliojeruhika tunawaombea wapone haraka, tunaamini hekima ya Mungu itakuwa juu ya serikali yao kushughulikia jambo hilo kikamilifu.
Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai, hata sasa tunapoende kumalizia robo ya tatu ya mwaka 2013, tumeshuhudia mambo mengi sana mwaka huu ya kila aina, yapo yale yalionza kwa mara ya kwanza na mengine yamekuwa ni mwendelezo tu wa yale yadumuyo au yalioyaanza hapo kale, tumeshuhudia michezo mbalimbali na vipaji lukuki vikiinuka na kuimarika katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, na kwa yote mema na mazuri tunampa Mungu Utukufu kwa hakika!


UTANGULIZI JUU YA JOHN LISU;

John Lisu ni mmoja wa waimbaji/Waabudishaji wanaoheshimika katika Tasnia ya muziki wa Injili kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa katika kukuza na kuendeleza muziki wa Injili nchini Tanzania na nje ya Nchi. Nyimbo nyingi alizozitunga na kuziimba zimekuwa zikitumika katika makanisa mbalimbali kama nyimbo za kusifu na kuabudu; pia waimbaji wengine waliokua wakiimba naye wameweza kukua na kufikia uwezo wa kuwa waimbaji wa kujitegemea. John Lisu pia ametia hamasa kubwa miongoni wa wanamuziki wa Injili kuanza kufanya muziki wa live. John Lisu ameweza kufanya tours za ndani ya Tanzania, Africa na Bara la Ulaya kwa ajili ya huduma.
CHRISTINA SHUSHO

John Lisu anategemea kufanya Project II ya Live recoding inayojulikana kama "UKO HAPA" baada ya project ya kwanza ya Jehova yu hai kufanya vizuri sana. Tamasha litafanyika ndani ya ukumbi wa City Christian Centre (CCC) Upanga tarehe 6 Octoba 2013, kuanzia saa 8. mpaka saa 2 usiku.
PAUL CLEMENT

 Tamasha litasindikizwa na waimbaji nguli kama Christina Shusho, Neema Gospel Choir, Paul Clement, Pastor Safari Paul, Bomby Johnson Waimbaji wote wamethibitisha kuwepo. 

BOMBY JOHNSON

VENUE:
City Christian Centre (CCC) mkabala na chuo kikuu cha mzumbe
Si mbali saana kutoka Diamond Jubilee
MIRIUM LUKINDO WA MAUKI


USAFIRI (basi zilizobandikwa matangazo ya tamasha) utakuwepo kutoka posta mpya kwenda ukumbini kuanzia saa saba na nusu mchana kwa bei ya kawaida.
PASTOR SAFARI PAUL

HABARI NJEMA-MUHTSARI!!!!!

Sasa kwa mara pili nchini Tanzania, mwimbaji WA NYIMBO ZA INJILI na mwabuduji JOHN LISSU wa jijini Dar Es Salaam, atakuwa anafanya Ibaada kubwa ama Tamasha la kusifu la Kuabudu(LIVE PERFORMANCE), litakalorekodiwa moja kwa moja (DVD LIVE RECORDING) lenye jina “UKO HAPA” (Yaani Mungu na Uwepo wake).
Tamasha hilo litafanyika jumapili ya Tarehe 6, Octoba 2013  katika Ukumbi mkubwa wa kisasa wa Kanisa la City Christian Centre (CCC)- Upanga, mkabala na Chuo Kikuu Mzumbe – tawi la Dar es salaam, kuanzia saa nane mchana.
Tunataraji watu 5000 kuwa sehemu ya tamasha hili la kipekee,Utakuwa sehemu ya tamasha hilo kwa tiketi ya 10,000/= (kawaida), 20,000/= (VIP) na 3000/= (Watoto);
na Kwale watakaohitaji tisheti maalum za tukio hilo, basi zinapatikana kwa kati ya 12,000-15,000/=, wewe wasiliana tu na (0713905118)
NELLY-MKE WA JOHN LISU


VITUO VYA KUUZIA TIKETI;
1.   MWENGE – Tarakea duka la Kanda
2.   KINONDONI – DPC
3.   MLIMANICITY – Silverspoon Restaurant
4.   KARIAKOO – Mbogo Shop
5.   UKONGA BANANA – KWA GIDO
6.   POSTA - DUKA LA MSAMA

T-SHIRTS

-T-shirts maalumu kwa wanaume na wanawake zinapatikana katika vituo vya kuuzia tiketi kwa bei ya elfu kumi, mpaka elfu 15(kutegmeana na aina).

N.B; Kwa tiketi ya VIP, mnunuzi atajipatia na Audio CD ya John Lissu ya “Uko Hapa”

USAFIRI UTAKUWEPO!!
Siku ya tamasha kutakuwepo usafiri kutoka Posta Mpya mpaka CCC-Upanga,eneo la tukio, hivyo kama wewe ni mgeni na hupafahamu mahali hapo, basi utakachotakiwa kufanya ni kupanda magari toka ulipo mpaka posta mpya kabla ya saa nane,na hapo utayakuta mabasi yenye mabango ya Tamasha, basi utajongea humo na hapo utawezeshwa kufika eneo la tukio, muhimu ni kuzingatia muda!

MUHIMU SANA!!

JOHN LISU NA TIMU NZIMA WAKIWA MAZOEZINI


Tamasha hili ni muhimu sana kwa Tanzania, hasa ukizingatia JOHN LISSU ni mmoja wa waimbaji wa kwanza kuimba live kila mahali anapoalikwa na ni mwimbaji wa kwanza binafsi kufanya LIVE DVD RECORDING pale Ubungo plaza, na ile ya kwanza iliitwa “JEHOVA YU HAI” na sasa anafanya LIVE RECORDING kwa viwango vingine bora zaidi, maana Mungu hutupa hatua moja zaidi kila siku.
Ni muhimu kwa kila mtanzania kujivunia kipaji na tukio hili muhimu katika historia, njoo umwabudu na kumsifu Mungu pamoja, Njoo ujifunze, Njoo umuunge mkono mtanzania mwenzako na njoo uje ufanyike sehemu ya Historia hii kwa Utukufu wa Jehova.
NEEMA GOSPEL CHOIR-KWAYA PEKEE ITAKAYOSHIRIKI "UKO HAPA"


MWALIKO MAALUM;
Kipekee Ninapenda kuwakaribisha wachungaji, mitume, manabii, wainjilisti, waalimu na viongozi wote wa makanisa na huduma mbalimbali, ninawakaribisha viongozi wote wa kisiasa na kijamii kutoka serikalini na vyama vya siasa vyote, ninapenda kuwakaribisha wanaharakati na wanataaluma wote, ninapenda kuwakaribisha waimbaji wote wa nyimbo za injili na wanasanaa wote, ninapenda kuwakaribisa wanafamilia wote, asiwepo wa kubaki nyuma, ninapenda sasa kukukaribisha wewe unaesoma hapa, naam nisaidie kumkaribisha na mwenzako na yeye aje na mwenzake, kimsingi tukio hili ni letu wote bila kujali kitu chochote, njooni tumsifu na kumwabudu Bwana na Mungu hataacha kuibariki Tanzania!
EMMANUEL NDIYE ATAKAYEMPIGIA JOHN LISU LEADING GUITOR


SHUKRANI;
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Hakneel Production (Wadhamini wakuu), na Jonn Lissu na timu nzima ya maandalizi; Kanisa la CCC-Upanga; vyombo vya habari hususani Praise Power na WAPO Radio; Clouds TV kupitia CHOMOZA na Clouds Radio kupitia GT; Sibuka Tv kupita Gospel Hits; Bloggers hususani Christian Bloggers, magazeti na vyombo vingine vyote vya habari! Shukrani hizi zimfikie kila mtu mmoja mmoja aliyetoa mchango wa mawazo, fedha, ushauri, maombi, ubunifu, yaani mchango wowote wa hali na mali na Mungu awabariki nyote!
MIRIUM LUKINDO WA MAUKI


MUHTASARI MKUU;
Tukio; TAMASHA LA KUSIFU NA KUABUDU, LITAKALOREKODIWA
(DVD LIVE RECORDING CONCERT)
Mhusika; JOHN LISSU
Jina: “UKO HAPA”
Mahali; UKUMBI WA KANISA LA CITY CHRISTIAN CENTRE (CCC)- UPANGA
Lini; 06TH OCTOBA, 2013
Muda; KUANZIA SAA NANE MCHANA
Kiingilio; Tsh 10,000/= (kawaida); 20,000/= (VIP) na 5000/= (Watoto)

Wasindikizaji; CHRISTINA SHUSHO, MIRIUM LUKINDO, PASTOR SAFARI, BOMBY JOHNSON, NEEMA GOSPEL CHOIR-AIC Chang’ombe na PAUL CLEMENT.

Mengineyo; USAFIRI UTAKUWEPO TOKA POSTA MPAKA CCC-UPANGA na Unaweza kujipatia Tisheti pia.
Wahusika; WATU WOTE MNAKARIBISHWA!


UKIPATA HABARI HII USIACHE KUMSHIRIKISHA NA MWENZAKO, NAAMINI HAUTAKOSA TUKIO HILI MUHIMU LA KIHISTORIA KATIKA NCHI YA TANZANIA KWA UTUKUFU WA MUNGU!!





KWA PICHA NA TAARIFA ZAIDI;





MAWASILIANO:
O713 240 397 – JOHN LISU
0713 905 118 –PROSPER MWAKITALIMA – EVENT MANAGER
0713 883 797 - FREDY CHAVALA - PUBLICITY


Imetolewa na;
Fredy E. Chavala <King Chavala (MC)>
Publicity Manager
+255 713 883 797
On Behalf of The Organizing Committee